TASWIRA: ZIARA YA MBOWE JIJINI ARUSHA KUNANI WAFIWA NA KUFARIJI WAHANGA WA TUKIO LA BOMU KATIKA KANISA KATOLIKI ARUSHA
Katika mazungumzo yake Mh Mbowe aliwapa pole wote waliofikwa na janga hilo na kuwataka watanzania wote wawe watulivu huku vyombo vya dola vikifanya kazi yake lengo likiwa ni kuwapata wahusika na ijulikane hasa lengo lao kulipua bomu kanisani lilikuwa ni nini. Baada ya kutoka hopsitalini hapo Mbowe na msafara wake walielekea Elerai kuhani msiba mmojawapo.