ZANZIBAR WAFANYA HITMA YA MZEE KARUME LEO




Wananchi na Waumini wa Dini ya Kiislamu wakisoma Hitma Kumuombea Dua Rais wa 

kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume,katika Ukumbi wa mikutano wa 

Ofisi ya CCm Kisiwandui Mjini Zanzibar,ambapo kila ikifika siku kama hii wananchi kwa 

ujumla wao hukusanyika kuomba dua kama hii.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Dk.Jakaya Mrisho Kikwete,akisalimiana 

na wakuu wa Vikosi vya ulinzi alipowasili katika viwanja vya Ofisi ya CCM Kisdiwandui Mjini 

Unguja kuhudhuria katika Hitma ya Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid 

Amani Karume.


Wake wa Viongozi Wakuu wakiwemo na viongozi wa taasisi za Kinamama wakinyanyua 

mikono juu kumuombea dua  Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani 

Karume.katika kaburi lake huko CCM Kisiwandui mjini Zanzibar,baada ya kisomo cha Hitma leo


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Alhaj Dk.Ali Mohamed 

Shein,akisalimiana na wakuu wa Vikosi vya ulinzi alipowasili katika viwanja vya Ofisi ya CCM 

Kisdiwandui Mjini Unguja kuhudhuria katika Hitma ya Rais wa kwanza wa Zanzibar 

Marehemu Mzee Abeid Amani Karume


Mke wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Mama Fatma Karume,(kulia) akiwa na Wake wa 

Viongozi mbali mbali katika Hitma ya Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid 

Amani Karume,huko Ukumbi wa CCK Kisiwandui Mjini Zanzibar Leo.

Akina mama wa Kiislamu wa Mjini Magharibi Unguja wakijumuika na Viongozi wengine katika kisomo cha HItmaya Kumuombea Dua Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume,leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar

Popular posts from this blog

TASWIRA: UZINDUZI RASMI WA KAMPENI ZA CHADEMA KWA UDIWANI WA KATA NNE ZA ARUSHA

RAIS KIKWETE ASAIDIA KUENDESHA HARAMBEE KUCHANGIA WODI YA DHARURA YA WATOTO NA VIFAA VYAKE HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI