Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo Mama Salma Kikwete akipokea zawadi za kimila za kabila la Wafipa, wakati alipokutana na akina mama wa manispaa ya Sumbawanga kwenye ukumbi wa Manispaa hiyo tarehe 25.2.2013.
Akiwa amevalia vazi la asili la akina mama wa kabila la Wafipa, Mke wa Rais Mama Salma Kikwete anashiriki kucheza ngoma ya kabila hilo kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga tarehe 15.2.2013.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi ambaye pia ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizindua rasmi shina la wakereketwa la kikundi cha akinamama cha Upendo kilichoko katika makao makuu ya wilaya ya Kalambo katika mji wa Matai tarehe 26.2.2013. Akinamama hao wapatao kumi hujishughulisha na kazi ya kukamua mafuta ya alizeti.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete akipokewa kwa shangwe na wananchi wa mji wa Matai waliofurika katika eneo la soko jipya mjini hapo ili kushiriki katika sherehe ya kukabidhi pikipiki kumi kwa ajili ya watendaji wa vituo vya afya katika mikoa ya Rukwa na Katavi tarehe 26.2.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkabidhi funguo za pikipiki Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Ndugu Paza Mwamlima kwa ajili ya vituo vya afya vya mkoa huo katika jitihada za kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT). Pikipiki hizo zimetolewa na kampuni ya Waterrids.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amembeba mtoto Emma, mwenye umri wa miezi minne na nusu, mtoto wa Maria, ambaye alijeruhiwa kwa kukatwa mkono na watu wasiojulikana wakati walipovamia nyumbani kwake tarehe 10.2.2013. Maria ni mke wa tatu wa Bwana Gabriel Yohana ambaye siku ya tukio hakuwepo nyumbani kwa Maria wakati watu hao walipomvamia.
Mbunge wa zamani wa Kwela Ndugu Chrisant Mzindakaya akishiriki kucheza ngoma ya utamaduni ya kabila la Wafipa wakati Mke wa Rais Mama Salma Kikwete alipotembelea hospitali ya Mkoa wa Rukwa kwa ajili ya kukabidhi vifaa mbalimbali vya tiba vyenye thamani ya shilingi milioni mia saba.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, Mama Salma Kikwete akimkabidhi Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dr. John Gurisha vifaa mbalimbali vya tiba kwa ajili ya hospitali ya Mkoa wa Rukwa tarehe 26.2.2013. Vifaa hivyo vimeletwa nchini na Taasisi ya WAMA kwa kushirikiana na Kampuni ya Project C.U.R.E kutoka Marekani na vina thamani ya shilingi milioni mia saba.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete hayupo pichani akiongea na wanafunzi wa kike kutoka shule mbalimbali za sekondari katika Manispaa ya Sumbawanga waliokusanyka katika shule ya sekondari ya Mtakatifu Theresia tarehe 26.2.2013
‘Chopa’ iliyotumiwa na Lema ikitua viwanja vya Shule ya Msingi Ngarenaro muda mfupi kabla ya kuanza mkutano. Chopa hiyo ilizunguka anga la Jiji la Arusha kwa madoido ya aina yake, hususani katika Kata nne za Themi, Kimandolu, Elerai na Kaloleni, halikadhalika eneo la mkutano, huku ikimwaga vipeperushi vya kunadi kampeni za Chadema na wagombea wake. Blog hii ilishuhudia wananchi wakigombea vipeperushi hivyo vikitua chini. Sehemu ya umati wa wananchi wa Jijini Arusha waliojitokeza jana katika viwanja vya Shule ya Msingi Ngarenaro kuhudhuria Mkutano Mkubwa wa Chadema wa Uzinduzi wa Kampeni za kuwania Udiwani kwa Kata nne zilizoachwa wazi na madiwani waliovuliwa uanchama na Chadema zaidi ya miaka miwili iliyopita. Mbunge wa Arusha Mjini na Mjumbe wa kamati Kuu Chadema, Mh Godbless Lema akihutubia umati wa wananchi waliojitokeza katika uzinduzi huo. Mwenyekiti wa Chadema Wilaya, ambae pia ni Mwenyekiti wa BAVICHA Mkoa wa Arusha na Diwani wa Kata ya Levolosi, Mh Ephata Nanyaro...
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjmin William Mkapa baada ya kuwasili katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibadilishana mawazo na Marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjmin William Mkapa katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam. Mkurugenzi w...